
Watu wengi humu duniani wana abudu Mungu na miungu mbali mbali na kuamini itikadi tofauti ndio maana kuna mirengo tofauti ya watu ambao wote wanamuabudu mungu wanavyofahamu. Wakristo, waislamu, wahindi, wayahudi, wabudha na wengineo wanafuata kanuni na sheria tofauti zinazo elekeza jinsi wanavyo shiriki na kuabudu mungu. Wote wako sawa na wana huru ya kuabudu wanavyoamini. Katika dini yoyote ile kuna misimamo misingi, kwa mafano wakristo yao ni ufufuo wa Yesu Kristo, ya waislamu ni kumuabudu Allah na kuyafuata mafunzo ya Mtume Muhammad, na Wabudha yao ni ibada kwa Budha. Kwa haya yote kila mshiriki anaelekezwa kufuata kanuni za dini na kuishi kulingana na mila na desturi zilizotengwa. Dini zote pia zina mafundisho yanayopatikana katika vitabu takatifu, kwa mfano, ya wakristo ni Bibilia na ya waislamu ni Quran.
...wazazi na jamii kwa ujumla wanapaswa kuwa waangalifu sana kuhakikisha kuwa maimamu wana mafundisho sahihi katika misikiti na kuwaongelesha vijana wao mara kwa mara ili kuwaelezea na kuwaonyesha jinsi ya kufuata dini vyema.
Wafuasi wa dini yoyote ile huwa wanawaamini sana viongozi wao na hujaribu kufuata vile wanvyofunzwa mambo ya dini. Makasisi na maimamu hufunza watu dini katika shule ya jumali na kwenye madrasa kutoka utotoni hadi utu uzima, na watu wanakuzwa kuamini itikadi mbali mbali kuhusu jinsi wanavyofaa kuendesha maisha yao. Kwa kiasi kikubwa dini inasaidia sana katika mambo ya kulainisha jamii na kuhakikisha kuwa watu wote wanaishi kwa amani. Ila kuna watu pia wanoichukua dini na kuitumia vibaya ili kutekeleza matakwa yao kibinafsi yasiyo ambatana na maagizo ya vitabu takatifu na kuwapotosha wengi. Watu kama hawa huwa wanakarabati na kubadilisha mafundisho ya kidini na kueneza misimamo yasiyoambatanisha na vitabu takatifu. Kwa kweli, wahenga walisema kuwa msema pweke hakosi, watu kama hawa wenye misimamo mkali huwa wameshawishika vilivyo kuwa misimamo yao ndio ya kweli na uhakika. Wanajitahidi sana kuwatafuta watu ili kuwashawishi na kuwapotosha na itikadi duni zisizokuwa na misingi katika dini. Watu wenye misimamo mkali wanapatikana katika dini zote iwe wakristo, wabudha au waislamu.
Elfu huanzia moja na watu hawa wenye misimamo mkali kwa mara nyingi huwa wanapatikana na kufunzwa itikadi potovu na maimamu na makasisi waliokiuka sheria za dini. Kila chombo kwa wimbile na makasisi hawa wakijitahidi huwa wanapata wafuasi kiasi wanaoamini maagizo yao kwani kinolewacho hupata. Na katika dini ya Islam, maimamu wanaoeneza itikadi ghushi wameweza kuwashawishi haswa vijana kuungana nao katika kutekeleza vitendo vya kigaidi kwa kigezo ya jihad. Wanatumia aya mbali mbali za Quran kuhalilisha vurugu na ugaidi, na kwa vile hawa vijana wana amini viongozi wa kidini wanaingia katika vikundi vya ugaidi huku wameahidiwa vinono vya mbinguni baada ya kutekeleza matakwa ya viongozi wao. La kusikitisha ni kuwa hawa viongozi hutumia uongo ili kuwashawishi vijana kuwa na misimamo kali na kujiunga na vikundi hivi vya kigaidi na baada ya kula kiapo na kujiunga hawa vijana hawana hiari tena na hutumika vibaya. Mtu yeyote yule anaweza kudanganganyika na akakubali misimamo mkali, wazazi na jamii kwa ujumla wanapaswa kuwa waangalifu sana kuhakikisha kuwa maimamu wana mafundisho sahihi katika misikiti na kuwaongelesha vijana wao mara kwa mara ili kuwaelezea na kuwaonyesha jinsi ya kufuata dini vyema.